
KOROSHO
ni zao muhimu la biashara katika nchi yetu kwani linampatia mkulima
kipato na kuliingiza taifa fedha za kigeni zinazotokana na mauzo ya zao
hilo ndani na nje ya nchi. Kwa
kawaida miti ya mikorosho inastawi vizuri katika ukanda wa Pwani ya
Bahari ya Hindi. Zao hilo hapa Tanzania linalimwa na wakulima wadogo
ambao wana miti mikorosho kati ya 60 mpaka 80.
Mikoa inayolima korosho ni Mtwara, Lindi, Pwani, Tanga na Ruvuma katika wilaya ya Tunduru. Mikoa mingine ambayo imeanza kulima korosho kwa kiwango kidogo katika maeneo yenye hali ya hewa inayofaa kwa kilimo cha zao hilo ni mkoa wa Mbeya, Njombe, Iringa, Morogoro, Dodoma, na Singida.
Mikoa inayolima korosho ni Mtwara, Lindi, Pwani, Tanga na Ruvuma katika wilaya ya Tunduru. Mikoa mingine ambayo imeanza kulima korosho kwa kiwango kidogo katika maeneo yenye hali ya hewa inayofaa kwa kilimo cha zao hilo ni mkoa wa Mbeya, Njombe, Iringa, Morogoro, Dodoma, na Singida.
Uzalishaji
wa juu wa korosho katika msimu wa mavuno wa mwaka 1973/74 ulifikia tani
145,000 za korosho ambazo kwa sehemu kubwa zilisafirishwa kwenda India.
Magonjwa ni kikwazo
Mbali
na hayo zipo changamoto mbalimbali ambazo zinasababisha baadhi ya
wakulima kukata tamaa kwa mfano kuwapo kwa ugonjwa unaoshambulia zao
hilo.Mkoani Mtwara, kuna kituo
cha utafiti wa magonjwa yanayoshambulia zao hilo cha Naliendele ambacho
kinafanya utafiti ili kubaini magonjwa na wadudu waharibifu, na kutafuta
ufumbuzi.
Dk
Louis Kasuga ni mtafiti wa kituo hicho anasema ugonjwa wa Ubwiri,
ulionekana ni tatizo kubwa katika kilimo cha korosho. Katika Miaka ya
karibuni pia ugonjwa wa blaiti nao umeonekana kushambulia zaidi zao hilo
na kwamba hivi sasa magonjwa hayo yamepatiwa dawa za kudhibiti magonjwa
hayo.
Dk
Kasuga anasema tatizo lingine ni gugu tegemezi (dodder) ambalo limekuwa
likiota kwenye maeneo ya Mtwara, Lindi, Kilwa, Rufiji, Mkuranga,
Bagamoyo, Pangani, Tanga na Mkinga. Gugu hilo ni chanzo chake ni mbegu
iliyoota na kutegemea mmea mwingine kama miti ya mikorosho kustawi.
Utafiti
uliofanywa na Kituo cha Naliendele kwa kikishirikiana na Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam umethibitisha kuwa gugu hilo linastawi vizuri katika
ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi. Dk
Kasuga anasema mbali ya gugu hilo kushambulia mikorosho pia
linashambulia mazao mengine kama michungwa, miti ya membe, mimea
mingine.
Wakulima
wanatambua kuwapo kwa tatizo hilo, lakini uelewa kuhusu chanzo cha
tatizo hilo numekuwa ni utata na namna ya kudhibiti bado limekuwa ni
kitendawili.
“Gugu
hilo halina majani hivyo halina uwezo wa kujitengenezea chakula chake
chenyewe, kwa msingi huo huishi kwa kutegemea mimea mingine ili liweze
kupata chakula ikiwa ni pamoja na miti ya mikorosho,” anasema mtaalamu
huyo.
Gugu lapunguza uzalishaji
Anasema gugu hilo linadumaza na
kunyonya chakula cha mimea mingine na kwamba gugu hilo linaweza
kusababisha mmea kufa au kukauka. Dk Kasuga anasema gugu hilo linasambaa kwa urahisi zaidi kwa njia ya upepo, maji, ndege, na wanyama.
Anasema gugu hilo linapunguza uzalishaji wa korosho kwa asilimia 100 kwa sababu linategemea miti ya mikorosho kupata chakula.
“Hii
ni kwa sababu ya ushindani wa chakula, maji na jua naa gugu hilo
linakuwa na lina nguvu kubwa ya kunyonya maji na chakula kutoka katika
mti wa mkorosho, hali hiyo inapunguza kipato cha mkulima kutokana na
kushuka kwa mavuno ya korosho,” anasema. Anasema gugu hilo linasababisha umaskini wa kipato na chakula katika kaya na kupunguza kipato cha fedha za kigeni kwa taifa.
Anabainisha
kwamba mbegu za gugu tegemezi zinauwezo wa kukaa chini ya ardhi kwa
miaka kumi bila kupoteza uwezo wa kuota na hivyo linaonekana kuwa sugu. Kwa
mujibu wa tovuti mbali mbali, mbegu za gugu tegemezi ni ngumu kufa
kwani hata wanyama wakila na kutoa kinyesi zinauwezo wa kuota.
Dk Kasuga
anasema njia za kudhibni gugu hilo ni kutoa kambakamba zake kwa
kuzivuta, ingawa gugu hilo limekuwa likirejea kwenye mti uliopo karibu
na gugu. Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Pwani, Robinso Wanjara anasema uongozi
wa Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na kituo cha utafiti cha magonjwa ya
korosho kimewapa maelekezo maofisa kilimo ngazi za kata ili wakachungeze
ukubwa tatizo hilo.
“Tunaamini
kuwa wataalamu wetu tuliowatuma kwenda kwa wakulima watatuletea takwimu
sahihi na kuzipeleka kwenye kituo cha Naliendele kwa ajili ya utafiti
zaidi,” anasema Wanjara.
Anasema
kutokana na kuwapo kwa gugu hilo katika Mkoa wa Pwani, anasema kuwa
kiwango cha uzalishaji kimekuwa kikisuasua na kusabaisha wakulima kupata
mavuno kidogo.
“Katika
mkoa wetu huu wa Pwani zao tunalolitegemea kwa ajili ya biashara ni
korosho likifuatiwa na muhogo, matunda, na mbogamboga sasa
linavyoathiriwa na gugu hilo linasababisha Mkoa wa Pwani uathirike
kimapato,”amesema.
Wakulima wazungumzia gugu tegemezi
Niliweza kupata fursa ya kuzungumza na
baadhi ya wakulima wa zao la korosho kutoka katika Kijiji cha Malendego
kilichoko Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi juu ya namna wanavyolitambua
hili gugutegemezi na njia wanazozitumia katika kukabiliana nalo Mkulima
wa Kijiji cha Malendego wilayani Kilwa, mkoani Lindi, Omary Mtunyungu
anasema gugutegemezi limemuathiri kiuchumi na kwamba umasikini unabisha
hodi katika familia yake.
Mtunyungu anasema kutokana na hali
hiyo ametoa taarifa kwa wataalamu wa kilimo ili kupata msaada wa
ufumbuzi, lakini mpaka sasa tatizo halijatatuliwa.
“Inaonekana
idadi ya wataalamu wa kilimo ni ndogo kwa sababu sisi wa huku kijijini
hatufikiwi na huduma hiyo naomba serikali ijitahidi kuongeza idadi ya
wataalamu ili watusaidie jinsi ya kukabiliana na vikwazo vya kilimo hasa
magonjwa .
Mkulima
na mkazi wa Kijiji hicho cha Malendego, Mohamedi Mtauka anasema amekata
tamaa kuongeza kilimo cha zao hilo kwa kuwa gugutegezi limeathiri sana
mimea yake ya korosho na kusababisha kipato chake kushuka.
Asili
ya kilimo cha zao la korosho ni kutoka nchi ya Brazil iliyopo Amerika
ya Kusini na liliingizwa Tanzania katika karne ya 16 kutokea Msumbiji
ambako lilikuwa likilimwa na Wareno.
No comments:
Post a Comment