Sunday, February 24, 2013

RUANGWA WATOA SOMO KWA MASASI


Na Cosmas J. Pahala      
Asasi ya kiraia, Ruangwa Decision Foundation imetoa somo kwa asasi za kiraia wilayani Masasi kwa kuaandaa Siku ya marafiki Ruangwa, ambayo itaadhimishwa kila mwaka tarehe 20 Februari, ambayo imeanza kuadhimishwa mwaka huu.
Lengo la kuandaa siku hii ni kutoa fursa kwa wakazi na wadau wa Ruangwa popote walipo kukutana Ruangwa ili kutoa msukumo wa kimaendeleo. Maadhimisho hayo yanaenda sambamba na kufanya usafi maeneo mbalimbali, kutembelea na kutoa misaada kwa wagonjwa, kusaidia watoto walio katika mazingira magumu na kupanda miti.
Ruangwa Decision Foundation imeanzishwa hivi karibuni ikiwa na dhamira ya kutoa msukumo wa kimaendeleo katika maeneo makuu matatu ambayo ni Elimu (elimu ya awali na msingi), Kilimo na Mazingira. Katika utendaji kazi wake inaongozwa na Kauli Mbiu IBUA HOJA IJADILIWE.
Wafanyakazi wa asasi mbalimbali za kiraia Mjini Masasi wakizungumza na Masasi leo, wamesema kuwa hatua iliyofikiwa na Ruangwa Dicision Foundation imeonesha mwanga na njia kwa asasi za kiraia zilizopo mjini Masasi na na ukanda wa kusini nzima.
Wilaya ya Ruangwa ni miongoni mwa wilaya ambazo ziko nyuma kimaendeleo katika nyanja za elimu, kilimo, afya, kiuchumi na kijamii. Kwa hiyo, Ruangwa Decision Foundation imekuja wakati muafaka na ujio wake utaleta mapinduzi makubwa kimaendeleo.


No comments:

Post a Comment